Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, September 28, 2010

MWANAMKE APOKEA KIPIGO TOKA KWA MUMEWE BAADA YA KUPOKEA SIMU KWA NAMBA NGENI


Pamoja na wanaharakati mbali mbali kuendelea kupiga vita vitendo vya unyanyasaji kijinsia vinavyoendelea kuota mizizi hapa nchini,bado baadhi ya wanaume wameendelea kuendekeza mfumo dume kwa wake zao pamoja na kuonyesha ukati wa kutisha.

Katika tukio hililotokea usiku wa kuamkia septemba 28 mwaka huu mwanamke mkazi wa Ilala mtaa wa Mwanayanga mjini Iringa Bi.Faraja amenusurika kifo baada ya kupokea kipigo cha kutisha kutoka kwa mwanaume ambaye amekuwa akiishinaye kwa kile alichodai kuwa ni kupigiwa simu usiku na mtu ayesimtambua ambaye alimtaka kutoka nje ya nyumba hiyo ili wakutane nje.

Akizungumza huku akibubujika damu baada ya kupigwa na kitu kizito katika paji lake la uso na mwanaume huyo ambaye katili ,Faraja alisema kuwa akiwa amekaa ndani ya mumewe huyo ilpigwa simu kutoka kwa mtu asiyefahamika akimtaka wakutane nje na bila huruma mwanaume huyo alianza kutoa kipigo huku akidai kuwa mwanamke huyo ni malaya wa mkubwa pamoja na kutokuwa na uhakika wa namba hiyo.


Hata hivyo baada ya kumpiga na kumuumiza vibaya mtu huyo ambaye alikuwa amepiga simu alirudia tena kupiga simu na kuomba radhi kuwa amepotea namba na kuwa yeye yupo Arusha alikuwa anamka Faraja ambaye ni mtoto wake hivyo inaonyesha namba imekosewa

NA.http://www.francisgodwin.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...