Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, May 20, 2011

MAKAMU WA RAIS MGENI RASMI SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAUGU





Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Muuguzi mstaafu Jito Ramu, aliyekuwa mmoja kati ya wauguzi waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salam leo. Dkt Bilal alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo ya jinsi wauguzi wanavyofanya kazi kuhusu mishipa ya fahamu na Ubongo, kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Wauguzi Tanzania Tawi la Moi, Prisca Tarimo, wakati alipotembelea banda la Moi Dharura, kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salam leo.


Wauguzi wakipita na mabango yenye ujumbe mbalimbali mbele ya mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.


Baadhi ya wauguzi wakiserebuka kushangilia sherehehe hiyo wakati msanii wa muziki Mrisho Mpto, walipokuwa akitoa burudani kwenye sherehe hizo.


Wauguzi waliohudhuria sherehe hizo wakila kiapo mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati wa sherehe hizo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Bodi ya Udhamini baada ya sherehe hizo.
Baadhi ya wauguzi wakipia kwa maandamano mbele ya mgeni rasmi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...