Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, September 28, 2011

WARATIBU WA CHEFA-EA WATEMBELEA NHIF


Sekretarieti ya Mtandao wa Muungano wa Taasisi zisizo za kiserikali za Mifuko ya Afya ya Jamii Afrika Mashariki (CHEFA-EA) imeipongeza Serikali ya Tanzania kwa namna inavyosimamia huduma ya Mfuko wa Afya ya Jamiii (CHF) nchini.

Pongezi hizo zimetolewa jijini leo na Mratibu wa mtandao huo Bw. Allen Oginga alipokutana na Uongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika ziara fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Mfuko huo Kurasini.
Bwana Oginga amesema, Tanzania kupitia NHIF imepiga hatua kubwa kwa kuweka uhusiano wa karibu kati yake na mtandao wa CHEFA-EA, hali iliyodhihirishwa na uamuzi wake wa kutoa ofisi katika Makao Makuu yake kwa ajili ya shughuli za Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) na zile za Mtandao wa CHF tanzania (TNCHF) ambao ni wanachama wa CHEFA-EA.

Awali, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw Hamisi Mdee aliueleza ujumbe wa Sekretarieti hiyo kuwa Bima ya Afya iko tayari kushirikiana na taasisi mbalimali za kijamii ili kuhakikisha kuwa jamii inapata huduma bora za matibabu kupitia NHIF na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ambao kwa sasa unasimamiwa na NHIF.

Kuhusu walengwa wa huduma za Bima ya Afya, Bw Mdee amesema makundi mbalimbali yamekuwa yakijumuishwa na hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2011 zaidi ya watanzania milioni 5 walikuwa wanahudumiwa na NHIF kupitia Bima ya Afya na Mfuko wa Afya ya Jamii.

Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa CHEFA-EA Bw Gaston Kikuwi amesema, lengo la ziara hiyo ni kujifunza, kubadilishana mawazo, kujenga mahusiano pamoja na kuitambulisha sekretarieti ya mtandao huo.

Kikuwi amesema ofisi za mtandao huo zimehama kutoka Kampala na kuwa Jijini Arusha kuanzia mwezi Julai, 2011 na kwamba uzinduzi wake utafanyika kati ya mwezi Novemba na Desemba mwaka huu.

Mipango ya baadaye ya CHEFA-EA ni kuongeza uwigo wa wanachama washiriki ili kujumuisha nchi zote ziolizoko kwenye shirikisho la ukanda wa Jumuiya ya ushirikiano wa nchi za afrika mashariki.

CHEFA-EA ilianza shughuli zake mwaka 1998 kama jukwaa la majadiliano na baadaye kuwa Mtandao kamili mwaka 2001. Kwa sasa Tanzania, Uganda na Kenya ni wanachama wa mtandao huo.
Wakiwa kwenye Picha ya pamoja baada ya Mkutano kutoka kushoto ni Bi.Penina Odhiambo,Allan Oginga waratibu (CHEFA-EA) kutoka Nairobi-Kenya ,Bwn. Hamis Mdee Naibu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF,kidani Magwila Mratibu wa CHEFA-EA Tanzania,Bwn Rehan Athuman Afisa anayeshughulika na Mifuko ya Afya ya Jamii (CHF),Sister Rita mratibu wa CHEFA-EA Tanzania ,Dr.Mathias Sweya Meneja Miradi ya Afya wa NHIF,Dr.Lawrence Lekashingo,na Mwenyekiti wa VIBINDO na CHEFA-EA Bwn. Gaston kikuwi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...