Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, December 19, 2011

Malt imezindua kampeni mpya ‘ANGALIA KWA MAKINI’







PRESS RELEASE
For immediate release

Ndovu Special Malt yawaalika wateja kutazama kwa umakini.
Tarehe 19 Disemba, 2011 - Ndovu Special Malt imezindua kampeni mpya ‘ANGALIA KWA MAKINI’ na kuwaalika wateja wake “kuangalia kwa makini” kile ambacho kinaipa Bia ya Ndovu ladha nzuri na ya kipekee, na kuifanya iwe bia bora zaidi yenye kiwango cha kimataifa.
Ndovu Special Malt imekuwa chaguo la wanywaji wengi wa bia nchini Tanzania ikiwa ni bia pekee ya kitanzania yenye hadhiya kimataifa.
Ndovu ilithibitishwa kuwa na kiwango cha kimataifa pale iliposhinda tuzo ya juu ya Grande Gold katika tuzo za Monde Grande Selection mwaka 2010. Tuzo hizi za “Grand Gold” hutolewa kwa bia zenye viwango vya ubora unaoazia asilimia 90 mpaka 100. Mpaka sasa tuzo hii imetolewa kwa Bia ya Ndovu pekee.
Ni nini kinachofanya Ndovu iwe Bia ya kipekee?
Meneja wa bia ya Ndovu, Pamela Kikuli alisema “Ndovu ina kiungo cha kipekee ambacho wanywaji wachache wa Ndovu wanakifahamu. Ni kimea angavu, Crystal Malt ambavu ambacho hakipatikani ndani ya bia nyingine hapa nchini. Kiungo hiki, crystal malt kimeandikwa kwenye nembo ya chupa ya Ndovu lakini watu wengi hawajaweza kutambua hilo. Kwa hiyo kwa kumsiadia mpenzi wa bia hii kufahamu kiungo hicho, kampeni mpya ya Ndovu ambayo tumeizindua hii leo inakusudia kumuwezesha mnywaji wa ndovu kutambua kiungo hiki kwa kutumia lenzi.
Gaudence Mkolwe, mpika bia mkuu wa kampuni ya Bia ya Tanzania (TBL) alisema “Crystal malt ni kiungo ambacho kiko ndani ya Ndovu na ndicho kinachoipa bia hii rangi yake ya dhahabu iliyokela na ladha laini ya kipekee. Hapa TBL tunajivunia sana kutengeza bia ya kiTanzania yenye ubora na tukiongelea ubora ni sawa na ubora wa kimataifa”
Natalia Celani, Meneja masoko wa Ndovu amesema “ Kampeni hii itatangazwa kwenye magazeti, mabango na kwenye baa mbalimbali hapa nchini. Pia kuna tangazo la redio linaloelezea jinsi kimea hiki kinavyoifanya bia ya ndovu kuwa ya kipekee, hivyo fuatilia kampeni hii na kama una lenzi tazama kwa umakini kwenye chupa ya Ndovu ili uone kiungo kinachoipa ladha ya kipekee bia hii”.


-ENDS-


For further Information
Pamela Kikuli Ndovu Special Malt, Brand Manager, pamela.kikuli@tz.sabmiller.com


2.

About TBL
Tanzania Breweries Limited (TBL) manufactures sells and distributes clear beer, alcoholic fruit beverages (AFB’s) and non-alcoholic beverages within Tanzania. TBL has controlling interests in Tanzania Distilleries Limited.

TBL’s most popular clear beer brands include Safari Lager, Kilimanjaro Premium Lager, Ndovu Special Malt, Castle Lager and Castle Lite, . Other prominent brands associated with the TBL group are Konyagi, Amarula Cream, Redds Premium Cold and Grand Malt.

The TBL group is listed on the Dar es Salaam Stock Exchange, employs about 1,300 people and is represented throughout the country with 4 clear beer breweries, a distillery, a malting facility and 9 distribution depots.



About SABMiller
SABMiller plc is one of the world’s largest brewers with brewing interests or distribution agreements in over 60 countries across five continents. The group’s brands include premium international beers such as Miller Genuine Draft, Peroni Nastro Azzurro, Grolsch and Pilsner Urquell, as well as an exceptional range of market leading local brands. Outside the USA, SABMiller plc is also one of the largest bottlers of Coca-Cola products in the world.

SABMiller plc is listed on the London and Johannesburg Stock Exchanges.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...