Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, June 26, 2012

Twiga Bancorp yashinda tuzo ya Dhahabu ya Utoaji Huduma bora duniani


 Afisa Mtendaji Mkuu wa Twiga Bancorp, Hussein Mbululo (kulia) akipokea Tuzo ya utoaji bora wa huduma  ijulikanayo kama ‘Century International Gold Quality ERA Award’, kutoka kwa Rais na Afisa mtendaji mkuu wa taasisi ya Kimataifa ya Business Initiative Directions, Jose Priento mjini Geneva-Uswisi. Twiga Bancorp imepata tuzo hiyo,kwa utoaji huduma zinazoridhisha kwa wateja, Uongozi bora, Mipango mkakati inayokidhi haja ya wateja  kama inavyotambulika katika QC 100 TQM.
 
Hivi karibuni Benki hiyo ilitunukiwa Tuzo ya Dhahabu iliyotolewa na jijini Geneva Uswis, tuzo hiyo inajulikana kama Century International Gold Award (ERA).
Lengo la tuzo hiyo ni kutambua ubora wa huduma zitolewazo kwa wananchi na taassisi au kampuni mbalimbali lengo lokiwa ni kuhamasisha utolewaji wa huduma bora kwa wateja.
Mtendaji Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, Hussein Mbululo amesema  kwamba Benki yake ilikuwa miongoni mwa Benki 100 zilizoshinda katika tuzo hizo kutoka nchi 47, tuzo hizo ziligawanywa katika makundi saba.
Amesema kujituma miongoni mwa wafanyakazi katika kuwahudumia wateja pamoja na ubunifu ndio siri kubwa ya mafanikio. 
Twiga Bancorp ni Benki inayo milikiwa na serikali ya Tanzania kwa asilimia mia moja (100%). 
 
Afisa Mtendaji wa Twiga Bancorp, Hussein Mbululo akiwa na baadhi ya maofisa wa BID mjini geneva kabla ya kuanza utoaji Tuzo.
CEO wa Twiga Bancorp, Hussein Mbululo akisalimiana na Rais na CEO wa BID, Jose Priento mjini Geneva-Uswisi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...