Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, September 27, 2012

AZAM FC NA JKT RUVU KUANZA KUONEKANA KATIKA MECHI ZA SUPER WEEKEND NA SuperSport


Mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kesho inaingia raundi ya nne, ambapo kwa mechi za Super Weekend ambazo zitakuwa zikionyeshwa moja kwa moja (live) na kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini. 
Miongoni mwa mechi zitakazoonyeshwa na kituo hicho, mechi ya kwanza itakuwa ni kati ya Azam na JKT Ruvu Stars, itakayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ambayo itaanza saa 1 kamili usiku kwa viingilio vya sh. 3,000 mzunguko, sh. 5,000 kwa VIP C na VIP B wakati VIP A kiingilio kitakuwa ni sh. 10,000.
 
Jumamosi pia kutakuwa na mechi kati ya Simba na Tanzania Prisons, ambayo pia itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni na siku ya jumapili, Yanga na African Lyon zote za jijini Dar es Salaam, zitakutana katika uwanja huo huo kuanzia saa 11 kamili jioni.

Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam wenyewe utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar, mchezo utakaochezwa Oktoba 1, mwaka huu kuanza saa 10.30 jioni.
Na mechi ya mwisho ya Super Weekend itachezwa Oktoba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikizikutanisha Yanga na Simba kuanzia saa 1 kamili usiku.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...