Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, December 31, 2012

"NAFSI NI NYONGE" TUSAMEHEANE NA MAISHA YAENDELEE. KARIBU 2013 KWA UFANISI ZAIDI


Wapendwa ndugu, jamaa na marafiki popote pale mlipo,yamebaki masaa kadhaa kuuaga mwaka 2012, ambao kwa hakika ulikuwa na changamoto nyingi za kimaisha, dhoruba za hapa na pale wengi zilitukumba, lakini kwa kudra za Mwenyezi Mungu akatushika mkono akatuinua na maisha yakaendelea.

Binafsi mpaka dakika hii namshukuru Mungu nikiwa mwenye afya njema kabisa. Maisha ya sasa Wanadamu wengi wamekuwa dhaifu kwa mambo mengi, lakini Mungu ndiyo njia sahihi wa kumtumia katika sala zako kuyashinda majaribu na madhaifu ya Dunia. Yako mengi ambayo naweza nikayaandika hapa lakini bado yasitoshe pia. Nasema asanteni kwa ushirikiano wenu mkubwa kwa namna moja ama nyingine, kama kuna mahali nilikosea, tukakwaruzana kidogo basi "NAFSI NI NYONGE" Tusameheane na maisha yaendelee.

Tunahamia mwaka mwingine mpya kabisa 2013, basi na tuendelee na ushirikiano huu tuliokuwa nao kwa mambo mbalimbali yenye kujenga na kuleta tija katika maisha yetu, Mwaka 2013 uwe wa kuhakikisha kweli sote pia tumehamia kwenye mfumo wa kidijitali, tushauriane, tuelemishane tunyooshane njia iliyo sahihi ili kila mmoja kila wakati abaki nafsini mwake mwenye furaha daima, Pia tumtangulize Mungu kila wakati kwa kila jambo ili pia azidi kuzibariki kazi za mikono yetu daima.

Kwa Blogaz wenzangu, changamoto nyingi tumekumbana nazo 2012, ikiwemo tatizo kuu la KUKOPY NA KUPASTE.! Na nyinginezo nyingi tuzijuazo zinatusumbua kwa namna moja ama nyingine, basi ni nyema 2013 iwe ya kuzitafutia ufumbuzi, kama si kuzimaliza kabisa basi angalau tuendelee kuzipunguza ili kuzimaliza kabisa, huku suala la kujituma na ubunifu vikiwa ndio ngao kuu ya mabadiliko miongoni mwetu. Ushirikiano tuliokuwa nao umeonesha tuna uwezo mkubwa wa kuisadia jamii inayotuzunguka na hata serikali pia kwa namna moja ama nyingi, basi tusimame kidete kuhakikisha ushirikiano huu hauteteleki ama haupotei kirahisi, badala yake tuiimarishe zaidi kila kona.

Natoa shukurani za dhati kabisa kwa makampuni na wadau mbalimbali ambayo/ambao kiukweli yametoa mchango mkubwa kuhakikisha tunasonga mbele na libeneke hili , si vibaya nikiyataja makampuni hayo kuwa ni Serengeti Breweries Ltd, Airtel, Bayport, Msama Promotions Ltd, kampuni ya R&R, Dada Teddy Mapunda, Hoyce Temu, Blogaz wote (bila kinyongo) na wengine waliotupa hatua ya kusogea kwa namna moja ama nyingine, Mungu awabariki sana.

Asanteni 
Nawatakia heri ya sikukuu ya Mwaka mpya.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...