Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, April 13, 2013

Matapeli wamhujumu rais wa IBF nchini




Rais wa IBF/USBA, Onesmo Ngowi
MATAPELI wa kimataifa wanaoingilia barua pepe na akaunti nyingine za watu mbalimbali wamemvamia rais wa hapa nchini wa Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF/USBA), Onesmo Ngowi na kutumia jina lake kwa nia ya kuwatapeli fedha watu mbalimbali anaojuana nao.
Jina la Ngowi ambaye pia ni Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, (TPBC), limetumiwa na matapeli hao kutuma ujumbe wa barua pepe kwa watu mbalimbali anaowasiliana nao, wahusika wakijifanya ni Ngowi na kuomba msaada wa fedha.
Katika barua pepe mojawapo iliyotumwa kwa mwandishi, inaeleza Ngowi alikuwa akiomba msaada wa Euro 2,950 (Sh. milioni 6.2) ili kumuwezesha kujinasua na tatizo lililomkumba akiwa nchini Ugiriki; jambo ambalo Ngowi amelilaani na kuwatahadharisha watu anaojuana nao kuwa wawe macho na matapeli hao.
"Matapeli wanatuma akaunti yangu (ya email) na kuomba pesa kwa watu mbalimbali... mimi siko Ugiriki na wala sijamuomba mtu fedha. Tafadhali naomba usijibu meseji hizo," alisema Ngowi kuelezea utapeli huo ambao umeshawakuta pia watu wengi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...