Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, May 22, 2013

MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS


MOROCCO Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas). 

 Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett. 

 Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.

 Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda. Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia. 

 Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo; Mei 22 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 23 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 23 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 25 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 26 Saa 3 asubuhi Uwanja wa Karume MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari.

 Mkutano huo utafanyika kesho (Mei 23 mwaka huu) saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF. Boniface Wambura Ofisa Habari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...