Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, July 12, 2013

NATASHA AFUNGUKA KUHUSU KUOLEWA KWAKE!




MWIGIZAJI mkongwe wa maigizo na filamu Bongo, Suzan Lewis ‘Natasha’ ambaye pia ni mtangazaji wa Radio Times FM, anayetarajia kufunga ndoa kesho, amefunguka kuwa anaoelewa kwa ajili ya kustarehe na siyo kwenda kuzaa kama wengine wanavyofanya.

Akizungumza na mwandishi wetu, Natasha alisema kuwa katika maisha yake hakuna kitu anachokichukia kama kubeba mimba na umri alionao ndiyo kabisa hawezi kufanya hivyo bali atalea wajukuu tu.

“Kuolewa si lazima kuzaa, mimi nimeolewa kwa ajili ya ‘ku-relax’ na kufurahi maisha kwa mume wangu na si vinginevyo, wakati wa kuzaa umeshapita, namwachia Monalisa (mwanaye) sasa aendelee kuijaza dunia,” alisema Natasha.

Mwanamama huyo ambaye hivi karibuni alifanyiwa bonge la pati katika sherehe ya kuagwa ‘send-off’ katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar alisema kuwa anaiombea ndoa yake idumu miaka mingi, wafe wazikane

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...