Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, September 26, 2013

KARAMA NYILAWILA KUZIPIGA OCTOBA 20


 

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini karama nyilawila ambaye alishawahi kuubeba ubingwa wa dunia wa  WBF –middle weight  kwa kumpiga kreshnik qato Wa Czech republic, katika ukumbi wa Sparta arena, plaque na kutwaa ubingwa  huo ambao una hadhi kama aliokuwa nao francis cheka kwa sasa, ambao baadae aliupoteza ubingwa huo kwa kutoutetea kutokana na kukosa wadhamini wa kumsaidia kuutetea ubingwa wake huo, na kushawishika kucheza na francis cheka  katika pambano alilopoteza na kukaa kimya muda mrefu bila kucheza  pambano la ndani ya nchi.
Karama anategemea kupanda ulingoni  tena tarehe 20 ya mwezi wa kumi katika ukumbi wa ccm mwinjuma.Mwananyamala  kuzipiga na sado philemon katika pambano lililoandaliwa na  bigright promotion.akilizungumzia pambano hilo Ibrahim kamwe anaeleza kuwa maandalizi mpaka sasa yanaenda vizuri pindi yapo katika mazingira magumu kwa wale watakaocheza utangulizi wanajiandaa kiukataukata kwa ajili ya pambano hilo ambalo litakuwa na mapambano mengi ya utangulizi, ukizingatia hatujapata mdhamini wa kudhamini pambano hili ili liwe katika ubora unaotakiwa , lakini tunapambana na tutajitahidi  pambano lifanyike vema tuwatie moyo hawa mabondia wanaochipukia na kuusimamisha vizuri mchezo wetu wa masumbwi.Karama na mwenzie philemon wameshasaini makubaliano ya mchezo huo na wapo katika hali nzuri ya kimchezo.
 
 
 
na
IBRAHIM ABBAS KAMWE

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...