Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, February 12, 2014

WAZIRI PROF. MUKANGARA AFUNGUA KONGAMANO LA TISA LA CTO LA MABADILIKO YA MFUMO WA UTANGAZAJI WA ANALOJIA KWENDA DIJITALI (DBSF) JIJINI ARUSHA

 

 
 Waziri wa Habari, vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenela Mukangara akifuatilia hotuba mbalimbali katika ufunguzi wa Kongamano la 9 la uhamaji wa mfumo wa utangazaji kutoka analojia kwenda dijitali Afrika  2014 (DBSF)ulioanza leo jijini Arusha. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Shirika la Mawasiliano kwa nchi za Jumuia ya Madola (CTO), Tim Unwin akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Prof. John Nkomwa.

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Prof. John Nkomwa akizungumza.
Baadhi ya waalikwa ambao ni viongozi wa Vituo vya televisheni nchini Tanzania
 Baadhi ya wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi ya TCRA wakifuatilia mijadala katika kongamano hilo.
  Waziri wa Habari, vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenela Mukangara akifuatilia hotuba mbalimbali katika ufunguzi wa Kongamano la 9 la uhamaji wa mfumo wa utangazaji kutoka analojia kwenda dijitali Afrika  2014 (DBSF)ulioanza leo jijini Arusha. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Shirika la Mawasiliano kwa nchi za Jumuia ya Madola (CTO), Tim Unwin akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Prof. John Nkomwa.
Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy ambaye pia ndiye Mwendeshaji wa kongamano hilo, akiteta jambo na Mkurugenzi wa Utangazaji wa TCRA, Habbi Gunze wakati wa kongamano hilo leo.
 Katibu Mtendaji wa Shirika la Mawasiliano kwa nchi za Jumuia ya Madola (CTO), Tim Unwin akizungumza.

Waziri wa Habari, vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenela Mukangara akitoa hotuba kwa Niaba ya Makamu wa Rais wa Tanzania ambaye alipaswa kuwa mgeni rasmi.
 
Baadhi ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Waziri wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo jijini Arusha leo.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara akishikana mkono na Katibu Mtendaji wa Shirika la Mawasiliano la Jumuia ya Madola (CTO) Tim Unwin (kulia) baada ya Waziri Mukangara kufungua kongamano la tisa la mabadiliko ya mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda Dijitali (DBSF) mjini Arusha jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma (katikati)
 Meza kuu katika picha mbalimbali za pamoja na washjiriki wote wa kongamano hilo la 9 la CTO na Uhamaji wa mfumo wa utangazaji kutoka analojia kwenda Dijitali
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara akisalimiana na Katibu Mtendaji wa Umoja wa mashirika ya Posta Afrika (PAPU), Younouss Djibrine (kushoto) baada ya Waziri Mukangara kufungua kongamano la tisa la mabadiliko ya mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda Dijitali (DBSF) mjini Arusha leo. Wengine ni Katibu Mtendaji wa Shirika la Mawasiliano la Jumuia ya Madola (CTO) Tim Unwin (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma (wapili kushoto)
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara akizungumza jambo na Katibu Mtendaji wa Shirika la Mawasiliano la Jumuia ya Madola (CTO) Tim unwin (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma (katikati)  baada ya Waziri Mukangara kufungua kongamano la tisa la mabadiliko ya mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda Dijitali (DBSF) mjini Arusha

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...