Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, March 18, 2014

Ngassa, Niyonzima warejea Yanga, Dida akiwakosa Azam


WAKATI winga machachari Mrisho Ngassa akianza kujifua na wenzake mjini Bagamoyo kwa ajili ya mechi yao ya kesho dhidi ya Azam, kipa tegemeo wa Yanga kwa sasa, Deo Munishi 'Dida' ataikosa mechi hiyo ya Ligi Kuu Tanzania Bara kutokana  na jeraha la mkono.
Kwa mujibu wa  Daktari wa timu hiyo, Juma Sufiani, Dida hatakuwamo katika kikosi chao cha kesho ingawa wachezaji waliokuwa wagonjwa,  Mrisho Ngassa na Haruna Niyonzima wenyewe wameanza kujifua.
"Niyonzima (Haruna) na Ngasa (Mrisho) wamerejea kikosini na wameshaanza kujifua lakini tutamkosa kipa Dida katika mechi yetu inayofuata kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya mkono," alisema Sufiani.
Niyonzima alikuwa anakabiliwa na malaria, huku Ngasa akisumbuliwa na majeraha ya nyama za paja na Twite (ruhusa).
Wakati Yanga hali ikiwa hivyo kuelekea kwenye mchezo wao wa kesho ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki kuona nani atakayemtambia mwenzake, wapinzani wao waliowafungwa mabao 3-2 katika mechi ya kwanza pia watawakosa wachezaji kadhaa ambao ni majeruhi.
Meneja wa Azam , Jemedari Said aliwataja wachezaji hao ni Haji Nuhu, Joseph Kimwaga ambao wanauguza magoti.
Jemedari alisema wachezaji wengine wote wapo fiti kwa ajili ya mechi hiyo ambayo wanahitaji kushinda ili kutimiza ndoito zao za kutwaa ubingwa baada ya misimu miwili wakiishia kukamata nafasi ya pili nyuma ya Simba na Yanga.
Azam, inaoongoza ligi hiyo kwa kuwa na pointi 43 baada ya majuzi kuifumua Coastal Union kwa mabao 4-0, huku Yanga ikikamata nafasi ya pili baada ya kuambulia sare na Mtibwa japo wanalinga pointi na Mbeya City waliopo nafasi ya tatu wakiwazidi mabao ya kufunga na kufungwa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...