Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, June 19, 2014

WARSHA YA TASAF ILIVYOZINDULIWA LEO NA WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS,MH.MOHAMMED ABOUD,ZANZIBAR

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud Mohammed, akifunguwa Warsha ya Kuwajengea Uelewa wa Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (PWP) katika mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini Tanzania, ilioandaliwa na TASAF Taifa. Iliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
 Mkurugenzi Uratibu wa Shughuliza Serekali Zanzibar, Ndg Issa Ibrahim Mahmoud, akitiwa maelezo ya Ufunguzi wa Warsha ya Kuwajengea Uelewa wa Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (PWP) katika mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini Tanzania unaotekelezwa na TASAF, uliofanyika katika ukumbib mdogo wa Baraza la Wawakilishi Chukwani. Kushoto kwake Mkurugenzi wa Program wa TASAF Ndg Amadius Kamagenge akifuatiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe Mohammed Aboud. Mohammed.



WASHIRIKI wa Warsha ya Warsha ya Kuwajengea Uelewa wa Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (PWP) katika mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini Zanzibar wakimsikiliza Mkurugenzi wa Program wa Tasaf Ndg. Amadius  Kamangenge, akitowa maelezo ya Mradi TASAF.wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo. Yaliofanyika katika ukumbi mdogo wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
 Mkurugenzi wa Program wa TASAF Ndg Amadius Kamagenge, akitowa maelezo ya Utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Ujenzi  ambayo pia itawanufaisha walengwa  wa mpango wa kunusuru kayacmasikini Tanzania.
Maofisa wa Mradi wa TASAF Tanzania wakifuatilia ufunguzi wa semina ya Utekelezaji wa Mradi Utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Ujenzi  ambayo pia itawanufaisha walengwa  wa mpango wa kunusuru kayacmasikini Tanzania. Wakati Waziri Aboud akifungua semina hiyo katika ukumbi mdogo wa baraza la wawakilishi chukwani Zanzibar.
 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Ndg. Ahmad Kassim, akitowa maelezo ya mafanikio ya Mradi wa Tasaf Zanzibar wakati wa ufunguzi wa Warsha ya kuwajengea Uelewa wa Utekelezaji wa Mradi wa (PWP) .
Maafisa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania TASAF,kutoka kushoto Ndg. Abass Saleh, Bi .Mary Kiula na Ndg. Geofrey Nyamwihula, wakijadiliana jambo wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Kuwajengea Uelewa wa Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (PWP) katika mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini Tanzania
Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud Mohammed, akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Warsha ya Warsha ya Kuwajengea Uelewa wa Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (PWP) katika mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini Tanzania, ilioandaliwa na TASAF Taifa. Iliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud Mohammed, akiwa katika picha na Maofisa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF) baada ya ufunguzi wa  Warsha ya Warsha ya Kuwajengea Uelewa wa Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi (PWP) katika mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini Tanzania, ilioandaliwa na TASAF Taifa. Iliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...